jeudi 15 août 2013

EGYPTE: LES MILITAIRES EGYPTIENS FONT LA HONTE DE L'AFRIQUE

Crime Incroyable: Une journaliste occidentale  reporter, contacter au Caire par la RFI, informe avec joie les carnages opérée par l'armée Egyptienne. C'est inhumaine, 
Demontra clairement la position dangereuse de l'occident elle se contente de dire que les Egyptiens sont soulagés apres les carnages de plus de 2000morts.

Zaidi ya Watu 2000 wauawa kwenye Machafuko nchini Misri
Miili ya Watu waliouawa wakati wa machafuko ya nchini Misri
Miili ya Watu waliouawa wakati wa machafuko ya nchini Misri
REUTERS/Amr Abdallah Dalsh

Na Lizzy Anneth Masinga
Raia wa Misri wameendelea tena hii leo na shughuli zao baada ya kuwepo kwa hali ya hatari usiku mzima baada ya Watu zaidi ya 500 kuuawa wakati Vikosi vya usalama vilipokuwa vikiwatawanya Waandamanaji wanaomuunga mkono aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, Mohamed Morsi.

Jeshi linalounga mkono Serikali ya mpito lilitangaza hali ya taadhari nchi nzima kwa kipindi cha mwezi mmoja na hali ya hatari jijini Cairo na majimbo mengine 13.

Muda mfupi baada ya kumalizika kwa muda wa hali ya hatari hii leo asubuhi, taa za kuongoza magari barabarani ziliwaka tena katika mitaa ya jiji la Cairo, na barabara zilizokuwa zimefungwa kwa majuma kadhaa na Wafuasi wa Morsi zilifunguliwa.

Wizara ya Afya ilitangaza kuwa Takriban Raia 300 wameuawa na kuongeza kuwa Wana kikosi wa usala 43 wameuawa.

Ghasia hizi ni mbaya zaidi kutokea, tangu zile za mwaka 2011 ambazo zilimuondoa aliyekuwa Rais wa Taifa hilo Hosni Mubarak, ambapo Chama cha Muslim Brotherhood kimesema kiwa Watu 2,200 wameuawa na zaidi ya 10,000 wamejeruhiwa.

Katika hatua nyingine Makamu wa Rais wa Misri,Mohamed El Baradei amejiuzulu akisema kuwa anafadhaishwa na namna ambavyo Watu wamekuwa wakipoteza maisha wakati matukio hayo yangeweza kuepukika.

Operesheni hizo zilizanza kwa Vikosi vya usalama vilipotumia Gesi ya kutoa machozi dhidi ya Waandamanaji waliokuwa wamekita Kambi kukemea mapinduzi dhidi ya Morsi.

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire