lundi 11 février 2013

Nyama ya farasi yauzwa barani Ulaya na kuzua hofu


Mawaziri wa Ufaransa

Mawaziri wa Ufaransa wanakutana katika kikao cha dharura kuzungumzia kugundulika kwa uuzwaji wa nyama ya farasi katika viwanda vya nyama nchini humo.

Hali hii imezua maswali mengi kuhusu umakini wa viwanda vya nyama vinavyofanya biashara hiyo na kuthibitisha ubora wa nyama barani humo huku mataifa yanayoathiriwa yakiwa pia ni Uingereza, Ufaransa, Sweden , Ireland na Romania.
Inahofiwa kuwa mataifa mengine 11 huenda yakaathiriwa na uingizwaji na uuzwaji wa nyama hiyo ikiwa hatua madhubuti hazitachukuliwa.
Waziri anayehusika na maswala ya vyakula nchini Ufaransa Guillaume Garot amesema kuwa lengo lake ni kuondoa nyama hiyo kwenye maduka yote nchini humo.
Wamiliki wa maduka makubwa nchini Ufaransa wameondoa bidhaa zenye nyama kwa hofu hiyo huku idadi ya wateja nayo ikipungua.
Mwezi uliopita, wakaguzi wa chakula nchini Ireland walitangaza kuwa walipata nyama ya farasi katika bidhaa mbalimbali katika maduka makubwa nchini humo.
Madkatari wanaonya kuwa nyama hiyo inaweza kuwa na madhara kwa binadamu kwa sababu ya chanjo inayotumiwa kuwachanja farasi hao.
tags: Romania - Ufaransa - Uingereza

Aucun commentaire:

Enregistrer un commentaire