mardi 9 avril 2013

Wakenya waombe amani

 31 Machi, 2013 - Saa 14:49 GMT
Katika sala ya Pasaka mjini Nairobi rais mteule, Uhuru Kenyatta, aliwataka Wakenya waombe amani:
Uhuru Kenyatta
Bwana Kenyatta alisema:
"nachukua fursa hii kuwashukuru Wakenya wote kwa kuweka amani tangu kabla ya uchaguzi, wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi; na naendelea kuwaomba Wakenya kuomba amani, kwa sababu amani ndiyo itatupa uwezo wa kufanikiwa; na hiyo amani ndiyo itatuwezesha sote kufikia ndoto zetu, malengo yetu na matumaini ya Wakenya wote, popote walipo."

Huku nyuma polisi walipambana na waandamanaji wachache mjini Kisumu kwenye wafuasi wengi wa Raila Odinga ambaye Jumamosi alikataliwa malalamiko yake kuhusu matokeo ya uchaguzi wa rais, ambapo Uhuru Kenyatta alishinda.
Ghasia zilizotokea Jumapili ni ndogo tu baada ya ghasia za Jumamosi usiku, ambapo watu wawili walikufa mjini humo.
Inaarifiwa ghasia za Jumapili ni katika vitongoje tu vya Kisumu na polisi wanasema hali imedhibitiwa.

Bwana Odinga alisema Jumamosi usiku kwamba anaheshimu uamuzi wa mahakama, lakini ataangalia njia nyengine za salama za kutafuta suluhu.
Aliwaomba wafuasi wake waepukane na umwagaji damu.

Taarifa zinazohusiana

Afrika Kusini yatuma wanajeshi Congo

 8 Aprili, 2013 - Saa 06:04 GMT
Wanajeshi wa Afrika Kusini
Afrika Kusini imetangaza kuwa itatuma wanajeshi Jamhuri ya Demokrasi ya Congo kujumuika katika kikosi maalumu cha Umoja wa Mataifa cha kuingilia kati nchini humo ili kuwanyan'ganya silaha wapiganaji.
Taarifa hiyo imetolewa majuma machache tu baada ya wanajeshi 13 wa Afrika Kusini kuuwawa Jamhuri ya Afrika ya Kati katika hali ya kutatanisha.
Upande wa upinzani umelaani mpango huo, wanasema kuwa haukufikishwa mbele ya bunge.
Waziri kivuli wa Ulinzi wa chama cha Democratic Alliance, David Maynier, alisema kuna hatari ya wanajeshi zaidi kupoteza maisha yao.

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilitoa idhini mwisho wa mwezi uliopita kutuma kikosi kitachoweza kupigana na kuingilia kati katika Congo.

Taarifa zinazohusiana

Kumbukumbu za mauaji ya Kimbare Rwanda

 8 Aprili, 2013 - Saa 07:46 GMT
Mmoja wa washukiwa wawakuu wa mauaji ya Kimbare Leon Mugesera
Wanyarwanda wanaanza wiki ya kumbukumbu ya mauaji ya Kimbari ikiwa ni miaka 19 sasa tangu yatokee.
Na katika juhudi za kuponya nchi, Rwanda imekua na nguzo za kuleta maridhiano pamoja na mfumo wa sheria kuwajibisha waliohusika.
Licha ya juhudi hizi bado waathirika wengi wangali kupona mafadhaiko kutokana na mauaji hayo na sasa juhudi zimeanza kuwanusuru raia dhidi ya matatizo ya kiwewe.
Mwaka huu wanyarwanda wanakumbuka siku hii kwa kauli mbiu ya ''Tukumbuke mauaji ya kimbare dhidi ya Watusti tukijitahidi kujenga nchi yetu.''
Kinyume na kumbukumbu za hapo nyuma, ambapo watu walikusanyika katika uwanja wa kitaifa wa Amahoro wakati huu sherehe zitafanyika katika maeneo ya vijijini.
Ni miaka 19 tangu mauaji hayo kufanyika na wanyarwanda wanajaribu kuyasahau mauaji mabaya zaidi kuwahi kushuhudiwa nchini humo mwaka 19994 ambayo yaliwaacha zaidi ya watu milioni moja wakiwa wameuawa
Shughuli za mapatano miongoni mwa waathiri wa wa mauaji ya kimbari
Hata hivyo nchi hiyo imeweza kujikwamua na kugeuka kuwa mmoja ya mataifa yanayokuwa kwa kasi kubwa barani Afrika.
Huku Rwanda ikiwa bado inawakumbuka waliofariki katika mauaji hayo, baadhi ya washukiwa wakuu wa mauaji yenyewe wangali mbioni
Rwanda imetoa vibali vya kukamatwa kwa washukiwa 130 kote duniani ambao wanaendelea kukimbia. Mmoja wao ni Felicien Kabuga, anayetajwa kama mfadhili mkuu wa mauaji hayo.
Wengine ni pamoja na Protais Mpiranya, Augustin Bizimana, Fulgence Kayishema, Pheneas Munyarugarama, Aloys Ndimbati, Ladislas Ntaganzwa, harles Ryandikayo, and Charles Sikubwabo.
Washukiwa wengine kama Leon Mugesera na Jean Uwinkindi, wamekamatwa na kurejeshwa Rwanda.
Rwanda pia imetoa vibali 27 vya kuwakamata washukiwa wakuu kwa nchi za kigeni na kufikia sasa washukiwa kadhaa wameshakamatwa.

Taarifa zinazohusiana

Margraret Thatcher ni nani?

 8 Aprili, 2013 - Saa 17:49 GMT
Bi Margaret Thatcher alikua mmojawapo wa wanasiasa mashuhuri wenye ushawishi mkubwa wa karne ya 20.
Alipoondoka madarakani aliwaachia warithi wake, siyo tu wa chama chake cha Conservative bali pia Leba ingawaje msimamo wake ngangari na mara kwa mara wa ubishi ulibainisha utawala wake wa kipindi cha miaka 11 kama Waziri mkuu.
Kwa mda wote wa uongozi ulishuhudia wapiga kura wengi wa kawaida wakifaidi vilivyo, mfano wa kuweza kununua nyumba za manispaa na vilevile kununua hisa katika biashara kabambe ambazo wakati huo ziligeuzwa kua za umma, kama British gas na shirika la simu za mawasiliano BT.
Lakini msimamo wake wa kupinga siasa za mashauriano ulimfanya aonekane kua mtu anayegawanya na hili likasababisha sera zake na mfumo wa uongozi wake kupinga na hatimaye kupelekea wanachama wa chama chake waanze kumpinga moja kwa moja na ghsia kuzuka mitaani.

Ushawishi wa baba

Margaret Hilda Thatcher alizaliwa tarehe 13 October 1925 huko Grantham, Lincolnshire, babake Alfred Roberts, muuza duka la rejareja na mamake, Beatrice.
Babake akiwa mhubiri wa kimethodisti na diwani wa eneo ambaye alimshawishi mno binti yake Margaret na hata kurithi sera zake.
Aliwahi kunukuliwa akisema "kweli, bila shaka namshukuru sana babangu kwa yote. Kweli alinilea na kunifanya niamini yote ninayoyatenda."
Margaret Thatcher alisomea masomo ya sayansi kutoka chuo cha Somerville College, Oxford, na kutokea kua mwanamke wa tatu kua RAIS wa shirika la wanafunzi wafuasi wa chama cha conservative.
Margaret na Mumewe Denis
Baada ya kuhitimu alihamia huko Colchester alikofanya kazi katika kiwanda kinachotengeneza plastiki na wakati huo huo akishiriki harakati za chama cha Conservative.
Mnamo mwaka 1949, alipendekezwa kama mgombea wa kiti cha mwakilishi wa chama chake cha huko Dartford wilaya ya Kent na licha ya juhudi kali alishindwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 1950 na 1951.
Hata hivyo aliweza kuweka pengo kwa kupunguza idadi ya wafuasi wa chama cha Leba kama mgombea mdogo kwa umri kutoka chama cha conservative aliyevutia mno vyombo vya habari.
Katika mwaka 1951 alifunga ndoa na mfanya biashara Denis Thatcher, na baada ya hapo kuanza somo la sheria. Alifuzu kama mwanasheria mwaka 1953, mwaka ambamo mapacha wake Mark na Carol walizaliwa.
Alijitahidi bila mafanikio achaguliwe kama mgombea mnamo mwaka 1955 na hatimaye akafanikiwa kujiunga katika bunge kupitia kiti cha conservative cha Finchley wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 1959.
Miaka miwili baadaye aliteuliwa kama waziri mdogo na kufuatia kushindwa kwa chama cha Conservative mnamo mwaka 1964 alipandishwa na kua Waziri kivuli.

'mwizi wa maziwa'

Kiongozi wa wakati huo wa chama Sir Alec Douglas-Home alipojiuzulu, Bi Thatcher akampigia kura Ted Heath katika kinyanganyiro cha mwaka 1965 cha kiongozi mpya na kuzawadiwa wadhifa wa msemaji wa masuala ya makaazi na ardhi.
Alipigia debe haki ya wapangaji wa nyumba za umma kuruhusiwa kuzinunua nyumba hizo na alikua msumari uliokosoa vikali sera za Leba za kodi ya kupindukia.
Ted Heath aliposhinda madaraka na kua Waziri Mkuu mnamo mwaka 1970 aliteuliwa kuiwa Waziri wa elimu kwa maelezo ya kupunguza matumizi ya wizara hio.
Mojapo ya hatua zilizotokana na hilo ni kuondoa mpango wa maziwa ya bure kwa wanafunzi walio kati ya umri wa miaka saba na kumi na mmoja. Hili lilizusha hujuma za chama cha Leba na vyombo vya habari vilivyombandika jina "Margaret Thatcher, milk snatcher" yaani mwizi wa maziwa.
Yeye binafsi alijaribu kupinga uwamuzi wa serikali wa kuondoa maziwa ya bure kama alivyoandika baadaye, nilijifunza somo muhimu. Nilifaidi shutuma kali za kisiasa bila faida yoyote kisiasa."
Akiwa mmoja wa kina mama wachache katika siasa za Uingereza, kulikuwa na fununu kuwa huenda siku moja akawa Waziri mkuu. Tetesi kama hizo zilimzunguka pia aliyekua Waziri katika chama tawala cha Leba Bi.Shirley Williams.
Margaret akiwa shuleni
Lakini kama wanasiasa wengine Bi. Thather alipuuzilia mbali madai hayo.
Katika mahojiano ya Televisheni Bi. Thather alisema haamini uwezekano wa kuwepo kwa Waziri Mkuu mwanamke katika maisha yake.
Kutokana na matatizo mengi, Serikali ya Heath haikudumu kwa muda mrefu.
Kutokana na kukumbwa na mgogoro wa mafuta wa mwaka 1973, uliopelekea kupunguza siku za kazi kua tatu kwa wiki nzima halikadhalika mgomo wa wachimba mgodi, serikali ya Thatcher ilizidiwa na mnamo mwezi febuari mwaka 1974 iliachia madaraka.
Thatcher akapewa wadhifa wa Waziri kivuli wa mazingira, lakini alikasirishwa na kile alichokiona kama sera za kigeugeu chini ya Bw.Edward Heath, akaamua kumpinga kwa kuwania uongozi wa chama cha Conservative mnamo mwaka 1975.
Alipokwenda afisini kwa Heath kumfahamisha uwamuzi wake, hakuhangaika hata kumtizama usoni. Alijibu kwa kejeli, utashindwa tu. Na kwaheri.
Kwa mshangao wa wengi, alimshinda Heath katika kura ya kwanza akimsababisha kujiuzulu na kumshinda Willie Whitelaw katika hatua ya pili na hivyo kujitokeza kua mwanamke wa kwanza kabisa kuongoza Chama cha siasa nchini Uingereza.
Moja kwa moja akaonyesha ujasiri wake. Hotuba yake ya mwaka 1976 iliyoshutumu sera za unyanyasaji za utawala wa Sovieti, ulisababisha gazeti moja la huko kumbadika jina la Iron Lady. Kwa kielelezo, Mwanamke mwenye msimamo wa chuma.Binafsi alifurahia jina hilo la utani.
Akitumia msimamo wa mama na mwanasiasa aliyefahamu machungu yaliyosababishwa na mdororo wa uchumi alivihujumu vyama vya wafanyakazi ambavyo hatua yao ya migomo ilisababisha hali mbaya wakati wa majira baridi mnamo mwaka 79.
Wakati serikali ya Bw. Callaghan ilipoanza kuyumbayumba, chama cha Conservertive kilichapisha vipeperushi vyenye kauli mbiu "Labour Isn't Working" yaani chama cha Labour kimeshindwa.
Jim Callaghan alishindwa katika kura ya maoni tareh 28 March 1979. Msimamo madhubuti wa Bi.Thatcher ulikubalika na wananchi wengi na kukipa chama cha Conservative ushindi katika uchaguzi mkuu uliofuata.

Sera ya Fedha

Akiwa Waziri mkuu alijitolea kurekebisha uchumi wa nchi kwa kupunguza mchango wa dola na badala yake kuimarisha soko huria.
Wajibu mkuu wa serkali ulikua ni kupunguza mdororo wa uchumi na punde si punde kuanisha mfumo wa kupunguza matumizi na bajeti.
Sheria zilibuniwa kupunguza malai ya vyama vya wafanyakazi, mashirika ya serikali kubinafsishwa na kuruhusu nyumba za manispaa ziuzwe kwa wananchi wanaoishi humo.
MaMilioni ya watu ambao hapo kabla hawakua na lao wala kumiliki chochote katika uchumi walijikuta wakiwezeshwa kumiliki nyumba zao binafsi na vilevile kununua hisa katika mashirika yaliyokua milki ya dola.
Margaret Thatcher
Sera mpya za fedha zikaufanya mji wa London kua mojapo ya miji iliyochangamka na vituo muhimu vya biashara ya kimataifa.
Mifumo ya kale ya viwanda ambayo wakosoaji wengi walilalamika kua imepitwa na wakati na kuweka taka la majengo ya viwanda, yaliondolewa kutoa nafasi katika juhudi za kuunda Uingereza mpya ya kisasa. Ukosefu wa ajira ulipanda kufikia milioni tatu.
Hili lilisababisha mvutano baina ya wanachama waliojulikana kama wets ama wabichi, na hilo pamoja na migomo katika maeneo mengi ya mji yalimzidishia Margaret Thatcher shinikizo za kumtaka arekebeshe sera zake.
Lakini Waziri Mkuu alikataa kutetereshwa. Aliuambia mkutano wa chama wa mwaka 1980: "kwa wale wanaongojea kwa pumzi nzito ya mageuzi kama magazeti yanavyopenda kuandika,nina jawabu moja kwenu. Mnaweza kugeuka mkipenda lakini Mama huyu si kugeuzwa.

Vita vya Falklands

Hadi mwishoni mwa 1981 umaarufu wake ulikua umepungua kufikia asili mia 25%, kiwango cha chini kwa Waziri mkuu yeyote hadi wakati huo lakini juhudi za kufufua uchumi zilikua zimepiga hatua.
Mapema mwaka 1982 Uchumi ulianza kunawiri na kunawiri huko kulimfanya Waziri Mkuu apande miongoni mwa wapiga kura.
Vita vya Falkland
Kiwango cha umaarufu wake kilipanda mno mwezi April 1982 kufuatia jibu lake kufuatia uvamuzi wa visiwa vya Falkland kutoka Argentina.
Bila kusita alituma kikosi cha wanamaji na visiwa kukombolewa tareh 14 Juni baada ya vikosi vya Argentina kusalimu amri.
Ushindi huko Falklands pamoja na mtafaruku katika chama cha Leba, kikiongozwa na Michael Foot, yalihakiki ushindi wa kishindo kwa chama cha Conservative katika uchaguzi mkuu wa mwaka 1983.
Utawala wake ulikumbwa na matatizo mengi, miongoni mwayo mizozo ya

Sera yake Afrika

Margaret Thatcher alimfedhehesha waziwazi Malkia Elizabeth juu ya sera yake juu ya ubaguzi wa rangi wa Makaburu wa Afrika ya kusini. Haya yalibainika alipokabiliana na viongozi wa Jumuia ya madola mwaka 1986 ambapo aliyekua Rais wa ZAMBIA Kenneth Kaunda alitaka Waziri Mkuu wa wakati huo atengwe kutoka mkutano huo wa viongozi.
Bi Thatcher alidai kua vikwazo dhidi ya Afrika ya kusini vingeathiri zaidi mali za Uingereza huko Afrika kusini na masdikini miongoni mwa raia wa nchi ho.
Alikubali Rais wa Afrika ya kusini PW Botha kuzuru Uingereza mnamo mwaka 1984 na kukitaja chama cha ANC kama kundi la kigaidi. Mwaka 1987 alisema kua yeyote anayeamaini kua Chama cha ANC kitaweza kutawala nchi hio kwa kauli yake anaishi katika sayari ya ndoto....Baadaye alikutana na Askofu Desmond Tut ingawa alikataa kukutana na Oliver Tambo. Mwaka 2006 David Cameron akiwa kiongozi wa upinzani aliomba radhi kwa sera yake juu ya Afrika kusini.
Katika mtazamo tafauti na hisia zake kuhusu chama cha ANC na Nelson Mandela, Margaret Thatcher alimsifu mno Robert Mugabe.
Baada ya kuhudhuria karamu aliyomuandalia mnamo mwaka 1982 alimsifu kwa tabia yake ya kirafiki na uwazi. Zimbabwe iliyofanikiwa bila shaka itachangia amani na utulivu katika Afrika ya kati na kusini mwa Afrika kwa ujumla, na tunakutakieni wewe na wenzako katika jitihada zenu, haya yamo katika maandishi yake binfasi.
Ingawa alikorofishana na Kenneth Kaunda mnamo mwaka 1986 uhusiano wao haukuwa wa uhasama. Katika juhudi ya kutafuta suluhu ,bw Kaunda alimualika wacheze densi wakati wa mkutano wa viongozi wa Jumuia ya madola uliofanywa mjini Lusaka mnamo mwaka 1979, Kaunda likumbusha katika mahojiano na BBC baadaye.
Aliitwa Iron Lady kutoka na usemi na msimamo wake
Bi Thatcher aliizurui Nigeria mara mbili. Akiwasili mjini Lagos mnamo mwaka 1988 alimvisha sifaa tele kiongozi wa kijeshi wakati huo General Ibrahim Babangida na kuelezea uwiyano uliopo baina ya Mataifa yao mawili. Hata hivyo ziara yake hiyo ililenga fungamano la mikataba ya biashara ya mafuta.
Wakati wa ziara yake hio alitembelea Kenya. Nigeria na Kenya zikionekana kama nchi zinazoipenda Uingereza. Baada ya kuchunguza miradi katika Rift Valley - na kuvishwa mauwa ya Kimasai Bi Thatcher akampaka sifa Rais Moi kwa muongozo wake wa amani na utulivu. Pia aliusifu moyo wa Harambee nchini Kenya akiulinganisha na sera za Uingereza.
Mwaka huo wa 89 alizuru Zimbabwe na Malawi na kutembelea Namibia bila kutarajiwa. Wadadisi wanasema kua ziara yake hio ilikua chachu ya kuanzisha mchakato wa Uhuru wa nchi hio.
Labda la kushangaza kwa nchi iliyokua chini ya utawala wa Kisoshalisti -raia wa Msumbiji walimpenda Iron Lady na kumfananisha na kiongozi wao shupavu Samora Machel.
Mwanawe Margaret Thatcher Mark pia alihusika mno na masuala barani Afrika - ingawa kwa hali ya kuaibisha. Mwaka 1982, alipotelea katika jangwa Sahara kwa mda wa siku sita wakati akishirtiki mashindano ya mbio za magari maarufu kama Dakar Rally.

Mwaka 2005 alikiri kua alivunja sheria zinazokataa mamluki nchini Afrika kusini kwa ununuzi wa ndege iliyotumiwa katika jaribio la kuipindua serikali ya Equatorial Guinea. Alipewa kifungo cha miaka minne nje ya jela.

Taarifa zinazohusiana

Man City yaitandika Man United 2-1

 8 Aprili, 2013 - Saa 21:29 GMT
Wachezaji wa Manchester City wakishangilia
Wachezaji wa Manchester City wakishangilia

Mabingwa watetezi wa taji la ligi kuu soka nchini England Manchester City,wameendelea kuwa na matumaini ya kutetea taji lao baada ya kuondoka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya watani zao wa jadi Manchester United kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Old Traford.

City ndio walikuwa wa kwanza kupata bao lao kupitia kwa James Milner kwa shuti la wastani baada ya makosa ya Ryan Gigs ambaye aliupoteza mpira ulio zaa bao hilo kunako dakika ya 51 ya mchezo.
Haikuwachukua muda mrefu United,kwani kunako dakika ya 59,United ilisawazisha bao hilo kupitia kwa Phil Jones kwa kichwa baada ya mpira wa adhabu ndogo iliyopigwa na Robin Van Persie na mpira huo kumgusa mgongoni nahodha wa Manchester City,Vincent Kompany.
Mechi hiyo iliyopigwa kwenye uwanja wa Old Traford,nyumbani kwa Manchester United,Ilishuhudia United wakionekana kuelemewa kimbinu na Man City ambao baada ya mabadiliko waliyoyafanya kwa kumtoa Samir Nasri na kumuingiza Sergio Aguero,Yalizaa matunda baada ya Muanjentina Sergio Aguero kuifungia timu yake bao la pili na la ushindi kwenye dakika ya 78,bao lililodumu hadi mwisho wa mchezo huo.
Manchester City inakuwa timu ya pili kuifunga Manchester United nyumbani kwenye mechi za ligi kuu msimu huu baada ya Tottenham Hotspurs kufanya hivyo mwezi Desemba mwaka jana.
Licha ya kufungwa,United itaendelea kuongoza ligi kuu ya England ikiwa na tofauti ya point 12 na Manchester City ambao wanakamata nafasi ya pili.
Mechi ijayo Manchester United itacheza na Stoke City siku ya jumamosi wakati Manchester City itasafiri hadi jijini London kucheza na Chelsea kwenye mchezo wa nusu fainali ya Michuano ya kombe la FA.

Tanzania yaiadabisha Morocco 3-1

 24 Machi, 2013 - Saa 16:42 GMT
taifa stars
Kikosi cha Stars kilichoanza dhidi ya Morocco,Picha kwa hisani ya mtandao wa Binzubery
Timu ya taifa ya Tanzania,Taifa Stars hii leo imeendeleza rekodi yake nzuri kwenye uwanja wa nyumbani baada ya kuitandika kwa jumla ya mabao matatu kwa moja timu ya taifa ya Morocco ambayo inaundwa na wachezaji wanocheza soka kwenye nchi za bara la Ulaya.

Tanzania ikiwa ni moja timu ya nne zinazounda kundi C barani Afrika,ikiwemo pia Ivory Cost,Morocco na Gambia zinazosaka nafasi ya kushiriki michuano ya kombe la dunia hapo mwakani nchini Brazil,Ilikuwa ya kwanza kupata bao la katika kipindi cha pili dakika ya 46,bao lililofungwa na Mshambuliaji wa kimataifa anayeichezea klabu ya TP Mazembe ya DRC,Thomas Ulimwengu aliyeingia akitokea benchi.

Wakiwa kwenye uwanja wa nyumbani wa Benjamini Wiiliam Mkapa,mbele ya mashabiki wao,Stars ilipata bao la pili dakika ya 67 kupitia kwa Mbwana Samata ambaye pia anaichezea klabu ya TP Mazembe na kuamsha shangwe kwa mashabiki wa soka wa Tanzania ambao wamekuwa na kiu ya zaidi ya miaka 30 ya kutoiona timu yao ya taifa ikishiriki michuano ya kimataifa tangu mwaka 1980 waliposhiriki kombe la mataifa huru barani Afrika iliyofanyika nchini Nigeria.

Mbwana Ally Samata,Mzaliwa wa Dar es Salam,mtoto wa Askari polisi wa zamani wa jeshi la Tanzania,aliiendelea kuwafurahisha watanzania baada ya kuandika bao la tatu dakika ya 80 na kufanya Taifa Stars kuiongoza mchezo huo kwa mabao matatu kwa bila kabla ya Morocco hawajazinduka na kupata bao la kufutia machozi lililofungwa na Yousef El Arabi anayeicheza klabu ya Granada ya nchini Hispania.

Dakika 90 zilimalizika kwa Tanzania kuibuka na ushindi wa mabao matatu kwa moja na kuwafanya kusalia kwenye nafasi ya pili wakiwa na point sita nyuma ya Ivory Cost ambao wana point saba wakiwa na tofauti ya point moja,ambapo Ivory Cost wao jana jumamosi waliwafunga Gambia kwa mabao matatu kwa bila.
Mechi ijayo Tanzania itasafiri hadi nchini Morocco hapo tarehe 6 mwezi wa sita mwaka huu kurudiana na Simba hao wa Milima ya Atlas ambao walipata kuwa mabingwa wa bara la Afrika mwaka 1976 katika Fainal zilizofanyika nchini Ethiopia.

MSIMAMO KUNDI C

NCHI MP W
D L F A PTS
1.COTE D`IVOIRE 3 2 1 0 7 2 7
2.TANZANIA 3 2 0 1 5 4 6
3.MOROCCO 3 0 2 1 4 6 2
4.GAMBIA 3 0 1 2 2 6 1

Idhaa

Dadis Camara attendu en Guinée

Dernière mise à jour: 9 avril, 2013 - 09:55 GMT
Le capitaine Moussa Dadis Camara à Ouagadougou en janvier 2010.
L'ancien chef de la junte militaire guinéenne, le capitaine Moussa Dadis Camara est attendu dans les prochains jours dans son pays.
Le capitaine Dadis, qui vit en exil au Burkina Faso depuis la tentative d'assassinat contre sa personne, va participer aux funérailles de sa mère décédée il y a quelques jours au Maroc.
Selon le porte-parole du gouvernement guinéen, Albert Damantag Camara, la décision de revenir en Guinée était une décision personnelle: “C’est une décision qui a été prise par le capitaine Dadis lui même. C’est la moindre des choses en matière de décès, surtout lorsque ça concerne un être si cher que la maman.
"Le gouvernement guinéen n’a eu qu’a prendre acte de cette décision, et je pense que c’est tout à fait naturel pour quelqu’un qui a servi ce pays et est un citoyen guinéen”, ajouté Albert Damantag Camara.

Restrictions de déplacement

Dans un premier temps, le gouvernement ne souhaitait pas le retour de l’ancien président guinéen.
Il a fallu une rencontre de la coordination de la Guinée forestière, la région d’origine du capitaine Dadis, avec le président Alpha Condé, pour que ce dernier accepte la venue de celui qui a dirigé la Guinée de décembre 2008 à décembre 2009.
En principe, Moussa Dadis Camara se limitera à visiter N'zérékoré, sa ville natale située en région forestière à plus de 1 000 kilomètres au Sud-est de Conakry, pour les funérailles de sa mère.
De nombreux habitants ne comprennent pas cette restriction imposée par les autorités.
Une restriction qui selon eux sous-entend que Dadis est bel et bien en exil forcé à Ouagadougou au Burkina Faso.
Aliou Bari, du parti d’opposition UFC, s’interroge: “je ne sais pas si Dadis lui même connaît ses droits, parce que à aucun moment, aucun papier ne dit que Dadis est assigné à résidence. Il a le droit non seulement de venir à Conakry, mais de partir à N'zérékoré”.

Mots-clés