lundi 30 septembre 2013

Watu 9 wauawa kaskazini mwa Burundi

Burundi - 
Makala iliyochapishwa tarehe : Thursday 21 julai 2011 - Taarifa za ivi karibuni : Thursday 21 julai 2011

Kanali Gaspard Baratuza, msemaji wa jeshi la Burundi
Kanali Gaspard Baratuza, msemaji wa jeshi la Burundi
Burunditransparence.org

Na Ali Bilali
Watu tisa wamedhibitishwa kaskazini mashariki mwa Burundi kufuatia mapigano kati ya polisi na watu wasiofahamika ambao walivamia eneo la mkoa wa kaskazini mwa Burundi wa Cibitoke.

Gavana wa Mkoa huo, Anselme Nsabimana amesema kuwa tukio hilo lilitokea siku ya jumanne asubuhi lakini kundi hilo la watu wasiofahamika waliendelea na mashambulizi dhidi ya polisi hadi jumatano usiku ambapo walifika eneo la tukio na kupata miili ya watu sita wakiwemo polisi wawili.
Msemaji wa jeshi kanali Gaspard Baratuza, amedhibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa polisi walifanikiwa kuwadhibiti wapiganaji wa kundi hilo ambapo hakuna taarifa rasmi kuwa kundi hilo ni la mrengo gani.
Hili linakuwa shambulio baya zaidi kuwahi kufanyika nchini humo tangu kumalizika kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo mwaka 2005.
Matukio kadhaa ya kuyumbishwa usalama yanaripotiwa mnamo siku zote hizi za nyuma tangu pale ulipomalizika uchaguzi wa bunge na rais uliokipa ushindi wa kishindo chama cha CNDD-FDD. Vyama vya upinzani vilipinga ushindi huo na kudai wizi wa kura ulifanyika.
vyama hivyo vya upinzani vilijiunga katika muungano unajumuisha vyama zaidi ya 10 na kuomba mjadala na serikali ya sasa ili kutatuwa matatizo yaliopo.
Serikali upande wake imekuwa ikitowa msimaloo wake kwamba haiwezi kuzungumza na chama chochote kuhusu maswala ya uchaguzi kwani kilipata ushindi, jhivyo kinauwezo wa kutumia ushindi huo kadri kitavyo.

Hali ikiendelea kuwa hivyo, uvumi umetanda kuanzishwa uasi. Dalili za uasi huo zimeanza kujionyesha baada ya matukio kadhaa, huku serikali ikikanusha kuwepo uasi bali makundi ya majambazi yanayo pora pesa na mali za wananchi.

Waasi 15 wa M23 na wanajeshi wanne wa serikali ya DRC wauwawa kufuatia mapigano mapya Kaskazini mwa Goma

DRC - 
Makala iliyochapishwa tarehe : Jumanne 21 mei 2013 - Taarifa za ivi karibuni : Jumanne 21 mei 2013

Wanajeshi wa serikali ya DRC
Wanajeshi wa serikali ya DRC
Presstv.ir

Na Sabina Chrispine Nabigambo
Waasi 15 wa M23 na wanajeshi wanne wa serikali ya DRC FARDC wameuwawa kufuatia mapigano mapya yaliyoibuka tena leo Jumanne huko Mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo  vyanzo vya kijeshi vimesema, siku moja kabla katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa kutembelea eneo hilo.

Kanali Olivier Hamuli, msemaji wa jeshi la Kongo (FARDC) katika jimbo la Kivu Kaskazini, amesema kuwa vikosi vya M23 vimeshambuliwa maeneo ya jeshi la serikali ya Congo FARDC katika eneo hilo hilo vililoshambulia jana Jumatatu, wakati mapigano yalipozuka kilomita 12 Kaskazini mwa Goma, mji mkuu wa mkoa .
Hamuli ameongeza kuwa wanafanya mashambulizi ambayo ni ya kwanza kushirikisha askari waasi wa M23 tangu mwezi Desemba.
Katibu Mkuu Ban Ki-moon atatembelea nchini DRC kesho jumatano katika ziara ambayo itamfikisha Goma pamoja na nchi jirani ya Rwanda na Uganda, ambayo serikali ya Congo na Umoja wa Mataifa inazituhumu kuwafadhili waasi wa M23 huku nchini zote mbili zikikanusha tuhuma hizo.

Mtaalamu wa kijeshi kutoka mataifa ya Magharibi amesema kuwa waasi wa M23 wanapambana kwa vinu na magari ya kivita yaliyotekwa kutoka majeshi ya serikali mwezi Novemba mwaka jana. Huku jeshi la serikali FARDC likitumia mizinga.

Mapigano makali yazuka nchini DRC kati ya Wanajeshi wa FARDC na Wapiganaji wa Kundi la M23

 
Jumamosi 20 julai 2013
Mapigano makali yazuka nchini DRC kati ya Wanajeshi wa FARDC na Wapiganaji wa Kundi la M23 kipindi hiki Marekani ikichungulia kuingia kwenye mgawanyiko wa kibaguzi wa rangi
Wanajeshi wa Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo FARDC wakiwa kwenye mapambano na Wapiganaji wa Kundi la Waasi la M23 huko Kivu Kaskazini
Wanajeshi wa Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo FARDC wakiwa kwenye mapambano na Wapiganaji wa Kundi la Waasi la M23 huko Kivu Kaskazini
REUTERS/Kenny Katombe
 
Na Nurdin Selemani Ramadhani
Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo FARDC limefanikiwa kuwadhibiti Wapiganaji wa Kundi la Waasi la M23 kwenye mapambano makali yaliyoshuhudiwa Jimboni Kivu Kaskazini na kuchangia dhidi ya wapiganaji wake mia moja ishirini na wanajeshi kumi wakipoteza maisha, Wananchi wa Misri wameendelea kugawanyika kwa misingi ya kisiasa kutokana na wafuasi wa Mohamed Morsi kuendelea kushinikiza Kiongozi wao arudishwe madarakani na kukataa kutambua mapinduzi yaliyofanyika, Rais wa Kwanza Mzalendo nchini Afrika Kusini na Mpambanaji dhidi ya Ubaguzi wa Rangi Nelson Mandela maarufu kwa jina la Mzee Madiba ametimiza miaka 95 alhamisi hii huku dunia ikienzi harakati zake na Taifa la Marekani huenda likatumbukia kwenye mgawanyiko wa rangi kutokana na wamarekani weusi kuoneshwa kukerwa kwa namna ambavyo hukumu zinatolewa na kuonesha kuna chembechembe za ubaguzi!!

Mapigano yazuka tena huko mashariki mwa DRCongo baina ya waasi wa M23 na vikosi vya serikali vya FARDC

DRCongo-mapigano - 
Makala iliyochapishwa tarehe : Thursday 22 agosti 2013 - Taarifa za ivi karibuni : Thursday 22 agosti 2013

Wanajeshi wa serikali ya Congo FARDC Julay 22 huko Kibati.
Wanajeshi wa serikali ya Congo FARDC Julay 22 huko Kibati.
REUTERS/Kenny Katombe

Na Ali Bilali
Mapambano makali yanaripotiwa tangu jana na leo baina ya waasi wa kundi la M23 na majeshi ya DRCongo FARDC kaskazini mwa mji wa Goma mashariki mwa nchi hiyo, duru za kijeshi kutoka katika mkoa wa Kivu ya kaskani zimethibitisha.

Kanali Olivier Hamuli msemaji wa FARDC kivu kaskazini mashariki mwa DRCongo azungumzia kuhusu mapigano na kundi la waasi wa M23 22 2013
 
22/08/2013
Mapigano hayo yalioanza jana jumanne jioni na kuendelea hadi leo alhamisi yanaripotiwa katika vijiji vya mutaho na Kibati kwenye umbali wa zaidi ya kilometa ishirini na jiji la Goma. Hakuna takwimu zozote ambazo zimetolewa kuhusiana na mapigano hayo.
Katika taarifa iliotolewa na kundi la waasi wa M23, kupitia msemaji wake Amani Kabasha, kundi hilo limelinyooshea kidole cha lawama jeshi la DRCongo FARDC kwa kuanzisha tena vita baada ya kushindwa juhudi za kidiplomasia wiki za hivi karibuni.
Kwa mujibu wa msemaji huyo wa M23, kuanzishwa tena kwa mapigano na jeshi la FARDC huko mashariki mwa DRCongo ni kuvunja mapendekezo ya viongozi wa kikao cha baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, pamoja pia na pendekezo la kikao cha viongozi wa ukanda wa maziwa makuu na kile cha Jumuiya ya kiuchumi cha viongozi wa nchi za kusini mwa Afrika SADC, walioomba kurejea kwenye meza ya mazungumzo huko Kampala nchini Uganda.
Kwa mujibu wa afisa mmoja wa jeshi la Congo ambaye hakutaka jina lake litajwe, amesema vikosi vya FARDC vilishambuliwa katika ngome zao vilivyokuwa vikikalia tangu mwezi uliopita kwenye umbali ta takriban kilometa ishirini na jiji la Goma. Hata hivo afisaa huyo hakutowa takwimu zozote kuhusu mapigano hayo.
Meja Modeste Bahati afisaa anaye husika na mawasiliano katika kundi la M23 amesema vikosi vya M23 vimebaki kwenye ngome zao, bila hata hivyo kutowa ufafanuzi zaidi.

Upande wake msemaji wa Jeshi la FARDC katika mkoa wa Kivu ya Kaskazini Mashariki mwa DRCongo Kanali Olivier Hamuli amesema, jeshi la FARDC ni jeshi la taifa, ninafanya juhudi zote kuhakikisha linawalinda wananchi na mali zao.

Mapigano mapya yazuka Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC

 
Jumamosi 24 agosti 2013
Mapigano mapya yazuka Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC huku shinikizo la kuchukunguzwa kama silaha za kemikali zimetumika nchini Syria likizidi
Wanajeshi wa Jeshi la Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo FARDC wakiwa kwenye doria katika Mji wa Goma kukabiliana na Kundi la Waasi la M23
Wanajeshi wa Jeshi la Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo FARDC wakiwa kwenye doria katika Mji wa Goma kukabiliana na Kundi la Waasi la M23
Reuters
Na Nurdin Selemani Ramadhani
Kikosi cha Umoja wa Mataifa Kulinda Amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo MONUSCO kimeamua kuingilia kati mapigano mapya yaliyozuka Mashariki mwa DRC kwa kutoa usaidizi kwa Jeshi la FARDC linalopambana na Kundi la Waasi la M23, Hali ya wasiwasi imeendelea kutamalaki nchini Misri kipindi hiki Kiongozi wa zamani wa Taifa hilo Hosni Mubarak akiachiwa kwa masharti huku Viongozi wa Chama Cha Muslim Brotherhood wakiendelea kushikiliwa na Mataifa ya Magharibi wamezidisha shinikizo kwa Serikali ya Syria kukubalia kufanyika kwa uchunguzi kubaini iwapo shambulizi lililotekelezwa kwenye viunga vya Damascus kama lilitumia silaha za kemikali!!

Mapigano yachacha Mashariki mwa DRC kati ya majeshi ya UN na waasi wa M 23


DRC - 
Makala iliyochapishwa tarehe : Thursday 29 agosti 2013 - Taarifa za ivi karibuni : Thursday 29 agosti 2013

Vikosi vya FRDC mjini Goma

Na Victor Melkizedeck Abuso
Mapigano mapya yamezuka Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kati ya majeshi ya serikali yakisaidiwa na yale ya Umoja wa Mataifa dhidi ya waasi wa M 23 karibu na mji wa Goma.

Wakaazi wa mji wa Goma wanasema wanasikia milipuko ya risasi mjini humo na watu hawatembei katika mji huo kama kawaida.
Mapigano haya mapya yanazuka siku moja baada ya mwanajeshi mmoja wa kulinda amani kuuliwa  na wengine watatu kujeruhiwa  katika makabiliano hayo.
Wiki hii, jeshi la serikali ya DRC likisaidiana na lile la Umoja wa Mataifa limekuwa likikabiliana na waasi wa M 23 katika eneo la Kibati karibu na mji wa Goma.
Kiongozi wa jeshi la kulinda amani MONUSCO Martin Kobler, amesema kuwa mwanajeshi aliyeuawa ni raia wa Tanzania na inaaminiwa alilengwa na kombora la waasi wa M 23 katika eneo la Kibati ambalo waasi hao wanasema ni ngome yao.
Aidha, Kobler ameongeza  kuwa mzozo wa Mashariki mwa nchi hiyo hauwezi kutatuliwa kwa matumizi ya nguvu za kijeshi na badala yake mazungumzo ya amani ya Kampala yanastahili kurejelewa ili kupata suluhu la kisiasa.
Msemaji wa Umoja wa Mataifa Farhan Haq amedokeza kuwa, kwa mara ya kwanza jeshi la MONUSCO limetumia ndege zake za kivita kukabiliana na waasi wa M 23 ambao wameonekana kujihami kwa silaha nzito.
Waasi wa M 23 wakiongozwa na kiongozi wao Betrand Bissimwa wanalishtumu jeshi la serikali kwa kuanza kuwashambulia katika ngome zao madai yanayopingwa na jeshi kupitia msemaji wake Mashariki mwa nchi hiyo Olivier Hamuli anayesema wao ndio waliovamiwa.
Mazungumzo ya amani kati ya serikali ya Kinsasha na waasi wa M 23 yamegonga mwamba jijini Kampala Uganda suala ambalo limeendelea kuhatarisha usalama Mashariki mwa nchi hiyo.
Mzozo wa Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo umekuwa ukiendelea kwa kipindi kirefu na ulizorota mwaka uliopita baada ya kuzuka kwa kundi la M23 lililodai kubaguliwa na serikali ya Kinsasha.

Serikali ya Rwanda imekuwa ikituhumiwa na jirani zao DRC na Umoja wa Mataifa kufadhili na kuwaunga mkono waasi wa M 23 tuhma ambazo Kigali imeendelea kukanusha.
Jeshi la kulinda la umoja wa Mataifa kutoka Tanzania, Malawi na Afrika Kusini tayari liko Mashariki mwa nchi hiyo kukabiliana na makundi ya waasi.

MONUSCO yaanza kuchunguza mauaji ya waandamanaji Goma


DRCONGO-MONUSCO - 
Makala iliyochapishwa tarehe : Jumatatu 26 agosti 2013 - Taarifa za ivi karibuni : Jumatatu 26 agosti 2013

Wanajeshi wa MONUSCO

Na Victor Melkizedeck Abuso
Jeshi la kulinda amani la Umoja wa Mataifa Mashariki kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo MUNUSCO, linasema  limeanza kuchunguza madai dhidi ya vikosi vyake kutekeleza mauaji ya watu wawili mjini Goma mwishoni mwa wiki iliyopita.

Kiongozi wa MONUSCO Martin Kobler, amesema kuwa jeshi hilo likishirikiana na lile la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo FRDC wameanzisha uchunguzi huo kubaini ukweli kuhusu mkasa huo.
Walioshuhudia mauaji hayo wanasema wanajeshi wa MONUSCO raia wa Uruguay waliwapiga risasi watu wawili wakati walipokuwa wanasambaratisha kundi la waandamanaji lililokuwa limevamia kambi ya jeshi hilo.
Mauaji haya yametokea siku moja tu baada ya kutokea kwa shambulizi la bomu  mjini Goma na kusabisha vifo vya watu watatu na pia kuwajeruhiwa wanajeshi watatu wa kulinda amani.
Wiki iliyopita, waasi wa M 23 na jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo wamekuwa wakipambana karibu na mji wa Goma huku kila upande ukituhumiana kuanzisha makabiliano hayo.
Ukosefu wa amani Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo umeilazimu serikali ya Uingereza kuwaagiza  raia wake wote wanaoishi na kufanya kazi mjini Goma kuondoka kwa kuhofia usalama wao.
Kiongozi wa kundi la M 23 Betrand Bissimwa amemwandikia barua Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon akilalamikia kuhusika kwa jeshi la kulinda amani katika mzozo wa Mashariki mwa nchi hiyo na kutekeleza mauaji .
Jeshi la serikali kwa upande wake linasema kuwa litaendelea kulinda mipaka ya nchi hiyo na pia kukabiliana na makundi ya waasi likiwemo la M 23 ikiwa litaanza kuwavamia.
Mazungumzo ya amani kati ya serikali ya Kinsasha na waasi wa M 23 yamegonga mwamba jijini Kampala Uganda suala ambalo limeendelea kuhatarisha usalama Mashariki mwa nchi hiyo.
Mzozo wa Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo umekuwa ukiendelea kwa kipindi kirefu na ulizorota mwaka uliopita baada ya kuzuka kwa kundi la M23 lililodai kubaguliwa na serikali ya Kinsasha.

Serikali ya Rwanda imekuwa ikituhumiwa na jirani zao DRC na Umoja wa Mataifa kufadhili na kuwaunga mkono waasi wa M 23 tuhma ambazo Kigali imeendelea kukanusha.
Jeshi la kulinda la umoja wa Mataifa kutoka Tanzania, Malawi na Afrika Kusini tayari liko Mashariki mwa nchi hiyo kukabiliana na makundi ya waasi.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ulinzi ya Kenya kumhoji Mkuu wa Usalama juu ya shambulizi la kigaidi kwenye Jumba la Biashara la Westgate


KENYA - 
Makala iliyochapishwa tarehe : Jumatatu 30 septemba 2013 - Taarifa za ivi karibuni : Jumatatu 30 septemba 2013

Jengo la Biashara la Westgate ambalo lilitekwa na kushambuliwa na Wanamgambo wa Al Shabab
Jengo la Biashara la Westgate ambalo lilitekwa na kushambuliwa na Wanamgambo wa Al Shabab

Na Nurdin Selemani Ramadhani
Maofisa wa Juu wa Usalama wakiongozwa na Mkuu wa Usalama wa Taifa nchini Kenya wanatarajiwa kuwa na wakati mgumu pale ambapo watakuwa wanahojiwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ulinzi wakituhumiwa kushindwa kufanyia kazi taarifa za kijasusi walizokuwa nazo juu ya kupangwa kwa Shambulizi la kigaidi katika Jumba la Biashara la Westgate. Mkuu wa Usalama wa Taifa atakuwa na kibarua cha kujibu ni kwa nini alishindwa kuwa na taarifa za kutosha ambazo zingesaidia kuzuia kutokea kwa shambulizi hilo la kigaidi linalotajwa kupangwa na kutekelezwa na Wanamgambo wa Kundi la Al Shabab wenye uhusiano na Mtandao wa Al Qaeda.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ulinzi nchini kenya imefikia uamuzi huo wa kumhoji Mkuu wa Usalama wa Taifa kutokana na uwepo wa taarifa zilizovuja na kueleza Kitengo cah Usalama wa Taifa kilikuwa na taarifa za kutokea kwa shambulizi hilo tangu mwaka 2011 lakini walishindwa kuchukua hatua madhubuti kulidhibiti.
Taarifa zimeendelea kuzagaa na kuanisha Kundi la Al Shabab lilishatoa tishio la kushambulia Jumba la Biashara la Westgate pamoja na Kanisa la Mtakatifu Bsilica lililopo Jijini Nairobi lakini hakuna hatua za haraka zilizochukuliwa kuhakikisha kitisho hicho kinafanyiwa kazi kwa wakati.
Vyombo vya Habari zimekuwa vikivujisha taarifa zinazoeleza kuwa Usalama wa Taifa wa Kenya ulivyopata taarifa hizo za onyo la kufanyika kwa mashambulizi walichukua hatua za kuifahamisha Marekani na Israel ili kuhakikisha wanawasaidia kuchukua hatua kukabiliana nalo.
Waziri wa Usalama wa Ndani wa Kenya Joseph Ole Lenku kwa upande wake amekanusha madai ya kwamba Serikali ilikuwa na taarifa zaidi ya mwaka mmoja kabla ya kutokwa kwa shambulizi hilo na kusema hizo ni taarifa zisizona ukweli wowote na kama wangepata onyo hilo wangelifanyia kazi.

Lenku amewaambia wanahabari Serikali imekuwa makani katika kuhakikisha wanaimarisha hali ya usalama katika nchi yote ya Kenya kwa hiyo wanapopata taarifa kama hizo hawawezi kukaa kimya kwani wanafahamu madhara yanayoweza kutokea ni makubwa.
Katika hatua nyingine Waziri Lenku amekanusha taarifa zilizokuwa zimezagaa ya kwamba zaidi ya watu sabini wamefukiwa kwenye vifusi vilivyochangiwa na kulipuliwa kwa jengo hilo na amesisitiza hakuna mtu mwengine aliyeuawa zaidi ya wale sitini na saba waliotolea maelezo.

Kumekuwa na taarifa na hali ya wasiwasi nchini Kenya kutokana na watu kadhaa kuendelea kusaka ndugu zao ambao hawajulikani walipo huku taarifa ya mwisho ya Shirika la Msalaba Mwekundu likisisitiza watu wanaokadiriwa kufikia sitini hawajulikani walipo.
Serikali nchini Kenya imesisitiza kwenye shambulizi hilo la kigaidi la huko Westgate walifanikiwa kuwaua Wanamgambo watano waliokuwa wamewashikilia mateka na kuwaua wananchi waliokuwa kwenye Jumba hilo.

Watu 39 hawajulikani walipo Nchini Kenya tangu kutokea kwa mkasa wa shambulizi la kigaidi katika Jumba la Biashara la Westgate


KENYA - 
Makala iliyochapishwa tarehe : Jumatatu 30 septemba 2013 - Taarifa za ivi karibuni : Jumatatu 30 septemba 2013

Jumba la Biashara la Westgate la Nchini Kenya lililoshambuliwa na Wanamgambo wa Al Shabab
Jumba la Biashara la Westgate la Nchini Kenya lililoshambuliwa na Wanamgambo wa Al Shabab
REUTERS/Thomas Mukoya

Na Nurdin Selemani Ramadhani
Shirika la Msalaba Mwekundu nchini Kenya limesema idadi ya watu waliokosekana tangu kutokea kwa shambulizi la kigaidi kwenye Jumba la Biashara la Westgate Jijini Nairobi imesalia kuwa watu thelathini na tisa tofauti na hapo awali ambapo watu sitini na mmoja walikuwa hawajulikani walipo. Shirika hilo limesema idafi hiyo imepungua baada ya watu kumi na nne kupatikana wakiwa hai huku miili mingine saba ya watu waliopoteza maisha kuendelea kuwepo kwenye vyumba vya kuhifadhia maiti kitu ambacho kimechangia kushuka kwa idadi ya watu waliokuwa hawajulikani walipo.

Wakuu wa Shirika la Msalaba Mwekundu nchini Kenya wamesema hadi kufika sasa hawana taarifa za watu hao thelathini na tisa licha a kwamba usafi wa kuondoa vifusi kwenye mabaki ya jengo la Westgate kufanyika kama ambavyo Jeshi nchini humo limethibitisha.

Taarifa hii ya Shirika la Msalaba Mwekundu inatolewa huku takwimu za Serikali zikiendelea kusalia watu waliopoteza maisha kwenye shambulizi hilo wakiwa ni sabini na saba wakiwemo wanasjeshi sita ambao nao waliuawa kwenye mashambulizi na wanamgambo wa Al Shabab.
Haya yanakuja huku Mkuu wa Usalama wa Taifa nchini Kenya akiendelea kuhojiwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ulinzi akituhumiwa kushindwa kufanyia kazi taarifa za kijasusi zilizokuwepo juu ya kupangwa kwa Shambulizi la kigaidi katika Jumba la Biashara la Westgate.

Mkuu wa Usalama wa Taifa ameendelea kukabiliwa na hali ngumu ni kwa nini alishindwa kuwa na taarifa za kutosha ambazo zingesaidia kuzuia kutokea kwa shambulizi hilo la kigaidi linalotajwa kupangwa na kutekelezwa na Wanamgambo wa Kundi la Al Shabab wenye uhusiano na Mtandao wa Al Qaeda.
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ulinzi nchini Kenya imefikia uamuzi huo wa kumhoji Mkuu wa Usalama wa Taifa kutokana na uwepo wa taarifa zilizovuja na kueleza Kitengo cah Usalama wa Taifa kilikuwa na taarifa za kutokea kwa shambulizi hilo tangu mwaka 2011 lakini walishindwa kuchukua hatua madhubuti kulidhibiti.

Taarifa zimeendelea kuzagaa na kuanisha Kundi la Al Shabab lilishatoa tishio la kushambulia Jumba la Biashara la Westgate pamoja na Kanisa la Mtakatifu Bsilica lililopo Jijini Nairobi lakini hakuna hatua za haraka zilizochukuliwa kuhakikisha kitisho hicho kinafanyiwa kazi kwa wakati.
Vyombo vya Habari zimekuwa vikivujisha taarifa zinazoeleza kuwa Usalama wa Taifa wa Kenya ulivyopata taarifa hizo za onyo la kufanyika kwa mashambulizi walichukua hatua za kuifahamisha Marekani na Israel ili kuhakikisha wanawasaidia kuchukua hatua kukabiliana nalo.

Waziri wa Usalama wa Ndani wa Kenya Joseph Ole Lenku kwa upande wake amekanusha madai ya kwamba Serikali ilikuwa na taarifa zaidi ya mwaka mmoja kabla ya kutokwa kwa shambulizi hilo na kusema hizo ni taarifa zisizona ukweli wowote na kama wangepata onyo hilo wangelifanyia kazi.
Lenku amewaambia wanahabari Serikali imekuwa makani katika kuhakikisha wanaimarisha hali ya usalama katika nchi yote ya Kenya kwa hiyo wanapopata taarifa kama hizo hawawezi kukaa kimya kwani wanafahamu madhara yanayoweza kutokea ni makubwa.
Katika hatua nyingine Waziri Lenku amekanusha taarifa zilizokuwa zimezagaa ya kwamba zaidi ya watu sabini wamefukiwa kwenye vifusi vilivyochangiwa na kulipuliwa kwa jengo hilo na amesisitiza hakuna mtu mwengine aliyeuawa zaidi ya wale sitini na saba waliotolea maelezo.

Kumekuwa na taarifa na hali ya wasiwasi nchini Kenya kutokana na watu kadhaa kuendelea kusaka ndugu zao ambao hawajulikani walipo huku taarifa ya mwisho ya Shirika la Msalaba Mwekundu likisisitiza watu wanaokadiriwa kufikia sitini hawajulikani walipo.
Serikali nchini Kenya imesisitiza kwenye shambulizi hilo la kigaidi la huko Westgate walifanikiwa kuwaua Wanamgambo watano waliokuwa wamewashikilia mateka na kuwaua wananchi waliokuwa kwenye Jumba hilo.

Nord-Kivu: 5 personnes tuées en une semaine à Beni par les soldats rwandais du M23

publié il y a 3 heures, 25 minutes, | Denière mise à jour le 30 septembre, 2013 à 12:50 | sous Actualité, La Une, Nord Kivu, Politique, Régions, Santé, Sécurité, Société. Mots clés: , , , ,

Ajouter une légende
La société civile de Beni accuse les rebelles ougandais de l’ADF-Nalu d’avoir tué cinq personnes et kidnappé trente-six autres, en l’espace d’une semaine, dans le territoire de Beni (Nord-Kivu). 

Dimanche 29 septembre dernier, ces rebelles ont enlevé trois personnes dans la localité de Maleki, à 10 km à l’Ouest de Oïcha, chef-lieu de beni (Nord-Kivu).
Selon des témoins, ces rebelles ougandais ont investi un centre de santé où ils ont emmené deux infirmiers, ligotés, vers une destination inconnue jusqu’à ce jour.

Avant d’enlever les infirmiers, ces ADF-Nalu ont brutalisé et intimidé les patients, semant un climat de panique dans le centre de santé de la localité de Maleki, indiquent les mêmes sources.
Un paysan a également été kidnappé le même jour par les mêmes assaillants, à 6 km du centre de santé de la localité de Maleki.
La société civile de Beni appelle les Forces armées de la RDC (FARDC) et la Monusco à une opération urgente de traque contre les ADF-Nalu qui ont accentué des exactions dans cette contrée.
Cette organisation citoyenne regrette que les militaires du 1er Secteur qui devraient sécuriser ce territoire soient pour la plupart déployées en Ituri (Province Orientale), laissant la population du territoire de Beni à la merci des groupes armés.

Le chef de la Monusco, Martin Kobler avait condamné, lundi 25 septembre dernier, «avec la plus grande fermeté» les attaques des groupes armés, particulièrement l’ADF, contre les écoles et les hôpitaux dans le territoire de Beni.
Lire aussi sur radiookapi.net:

La société civile du Nord-Kivu toujours opposée à l’intégration du M23 dans les FARDC

"Le gouvernement de Joseph Kabila payera très cher cette intégration des militaires rwando-ougandais du M23 dans la FARDC. Pour se maintenir au pouvoir, Kabila veut faire plaisir à Kagamé et Museveni en intégrant ces étrangers cruels dans notre armée. Pourtant il réconnait ke leur but final c'est la balkanisation de la RDC. Cela se retournera contre lui et son gouvernement."

publié il y a 6 heures, 35 minutes, | Denière mise à jour le 30 septembre, 2013 à 8:45 | sous Actualité, La Une, Nord Kivu, Sécurité. Mots clés: , ,

En avant-plan, Sulutani Makenga, le chef de la branche armée de la rébellion du M23 à Goma le 20 novembre 2012
Les grand criminels de guerres au KIVU
En avant-plan, Sulutani Makenga, le chef de la branche armée de la rébellion du M23 à Goma le 20 novembre 2012
Ads not by this site
Dans une lettre  adressée à Mary Robinson, l’envoyée spéciale du secrétaire général de l’Onu pour les Grands Lacs, et à Martin Kobler, représentant spécial du secrétaire général de l’Onu en RDC, la société civile du Nord-Kivu s’oppose à l’idée d’amnistier  et d’intégrer tous les rebelles du M23 dans l’armée tel que le propose le président ougandais Yoweri Museveni médiateur dans la crise entre Kinshasa et le M23.
 
 Une telle démarche est «dangereuse» pour le pays, estime la société civile dans cette correspondance publiée à Goma en début du week-end dernier.
«Notre coordination a appris la proposition du président ougandais d’une solution à la burundaise de la crise du M23. C’est-à-dire, l’octroi d’une amnistie générale à tous les éléments du M23 pour leur intégration ensuite dans les FARDC. Notre coordination attire l’attention  de Mme Mary Robinson et de M. Martin Kobler sur le danger que pareille initiative présente», a affirmé le porte-parole de la société civile du Nord Kivu, Omar Kavota.

D’après lui, «une intégration de ce genre consacrerait l’impunité flagrante des crimes de guerre, crimes contre l’humanité et d’autres graves violations des droits humains perpétrés par les criminels du M23».

Pour la population du Nord-Kivu, a poursuivi Omar Kavota, «la rébellion du M23 est composée des criminels, des militaires rwandais et ougandais qui cherchent à nouveau à infiltrer l’armée congolaise en vue de continuer à fragiliser la réforme de l’armée entreprise par le gouvernement et poursuivre le plan de la balkanisation.»

Il y a dix jours, Omar Kavota  avait exprimé sa «déception suite à la disponibilité du gouvernement congolais à intégrer les rebelles du M23 dans l’armée même dans les institutions politiques », estimant qu’en faisant cela, Kinshasa risquerait « d’intégrer au sein des FARDC une très grande partie de l’armée rwandaise».

Le gouvernement congolais a pour sa part remis à la Monusco une liste reprenant près d’une centaine de membres de la rébellion du M23 qu’il ne souhaite pas réintégrer dans l’armée.

Officiellement, les rebelles estiment que les questions liées à leur réintégration dans l’armée sont « subsidiaires ». C’est ce qu’a affirmé à l’AFP Bertrand Bisimwa, le président du M23 :
“Nous nous battons pour le pays et pour notre survie. Pour la sécurité de notre population, le retour des réfugiés et la réconciliation nationale. C’est à ces problèmes qu’il faut accorder beaucoup plus d’importance. Ces questions doivent trouver une réponse à Kampala. Nous ne nous battons pas pour l’amnistie, nous ne nous battons pas pour l’intégration. (…) La question de l’amnistie, la question de l’intégration, ce sont des questions subsidiaires.
Les dirigeants du M23 ont combattu au sein de l’ex-rébellion du CNDP avant d’intégrer l’armée aux termes d’un accord de paix signé le 23 mars 2009 à Goma avec le gouvernement. Le M23 tire son nom de cet accord de paix dont il revendique la pleine application depuis mai 2012.

En novembre 2012, les rebelles ont occupé brièvement la ville de Goma avant de la quitter en échange des négociations ouvertes en décembre de la même année à Kampala. Ces pourparlers suspendus depuis mai ont repris le 10 novembre dernier après que les FARDC appuyées par la brigade offensive de la Mission de l’Onu en RDC ont repoussé les rebelles à une trentaine de kilomètres de Goma qu’ils menaçaient de reprendre.
Lire aussi sur radiookapi.net:

jeudi 26 septembre 2013

Nord-Kivu: les FARDC tuent 2 rebelles du M23 à Kahunga

publié il y a 5 heures, 6 minutes, | Denière mise à jour le 26 septembre, 2013 à 1:31 | sous , , , , , , . Mots clés: , , , 

Les rebelles du M23 font leur entrée dans la ville de Goma, capitale provinciale du Nord-Kivu, mardi 20 novembre 2012.Les rebelles du M23 font leur entrée dans la ville de Goma, capitale provinciale du Nord-Kivu, mardi 20 novembre 2012.
Deux rebelles du M23 ont trouvé la mort, jeudi 26 septembre, au terme d’un accrochage qui les a opposés aux Forces armées de la RDC (FARDC), dans la localité de Kahunga, à près de 80 km au Nord de Goma (Nord-Kivu). Le porte-parole militaire au Nord-Kivu, lieutenant-colonel Olivier Hamuli, a indiqué qu’un militaire a été blessé au cours de ces échanges de tirs qu’il qualifie de provocation de la part du M23.

«Nous ne tolérerons plus une autre provocation de la part de ce mouvement rebelle», a prévenu le colonel Olivier Hamuli.
Cet accrochage à l’arme lourde et légère a été déclenché après que les rebellesont tenté de progresser vers la localité de Mabenga, sous contrôle des FARDC.
Après une vingtaine de minutes de résistance, les rebelles ont décroché et ils se sont dirigés vers la cité de Kiwanja, à 10 km du lieu de l’incident, laissant derrière eux deux cadavres, affirment des sources proches des FARDC.
Dans un communiqué parvenu à la presse, le président du M23 Bertrand Bisimwa, a plutôt accusé les FARDC de privilégier la guerre au détriment des négociations de Kampala. Ces pourparlers entre le gouvernement congolais et le M23 ont repris mardi 10 septembre dernier. Les deux parties attendent de la facilitation ougandaise un proposition d’accord.
Selon des sources concordantes, le M23 renforce actuellement ses positions aux environs de la localité de Mabenga, non loin de Kahunga, dans le territoire de Rutshuru (Nord-Kivu).
Lire aussi sur radiookapi.net:

RDC : l’armée a pris les « trois antennes », la forteresse du M23 à Kibati

août 30, 2013, | Denière mise à jour le 30 août, 2013 à 1:06 | sous , , , . Mots clés: , , , 

Les Forces armées de la République démocratique du Congo (FARDC) annoncent avoir délogé ce vendredi matin 
les combattants du M23 de la colline appelée « trois antennes », verrou stratégique des rebelles à Kibati. C’est depuis cette position située à une vingtaine de kilomètres de Goma que le M23 a lancé des mortiers sur les populations civiles dans le chef-lieu du Nord-Kivu.

La colline de « trois antennes » est tombée entre les mains des FARDC après des violents combats à l’arme lourde qui les ont opposées au M23, indiquent des sources concordantes à Kibati. D’après elles, les rebelles ont décroché après plusieurs heures de résistance.
Le colonel Olivier Hamuli, porte-parole de l’armée au Nord-Kivu, indique que les FARDC appuyées par l’artillerie de la brigade d’intervention de la Monusco ont mis en déroute les rebelles qui ont auraient pris la direction de Rumangabo. D’autres se seraient retranchés à Tchanzu sur les collines surplombant la cité frontalière de Bunagana, à l’Ouest de Kibati.
Les FARDC appuyées par la brigade d'intervention de la Monusco ont délogé vendredi 30 août 2013 le M23 de la colline de "trois antennes" à Kibati.Les FARDC appuyées par la brigade d'intervention de la Monusco ont délogé vendredi 30 août 2013 le M23 de la colline de "trois antennes" à Kibati.
Lors des combats de ce matin, les FARDC et les troupes de la brigade d’intervention ont détruit le principal dépôt d’armement des rebelles, souligne le colonel Olivier Hamuli. Pour l’instant, affirme-t-il, les FARDC appuyées par les casques bleus consolident leurs positions autour de la colline de “trois antennes” à Kibati.
C’est depuis cette colline que le M23a lancé jeudi et dimanche derniers des obus qui ont fait six morts à Goma. De nouveaux obus lancés depuis la même position a tué une personne jeudi dans la capitale provinciale du Nord-Kivu.
La RDC et l’ONU accusent le Rwanda d’armer les rebelles du M23. Ce que ce pays a toujours démenti. Jeudi, le conseil de sécurité a condamné dans ” les termes les plus fermes les attaques répétées et ciblées du M23 contre les civils et la Monusco”, dont un Casque bleu a été tué mercredi et plusieurs autres blessés.
Au cours d’une réunion du conseil de sécurité tenue jeudi à huis clos, l’ONUa dit détenir des “informations crédibles et cohérentes” sur un soutien de l’armée rwandaise aux rebelles du M23 dans les combats en RDC. Selon des diplomates qui ont assisté à cette séance, le Rwanda a bloqué mardi une proposition franco-américaine de sanctions contre deux responsables du M23. Il s’est aussi opposé depuis une semaine à plusieurs projets de déclaration du Conseil sur la situation à l’est de la RDC.
Martin Kobler, le patron de la Monusco s’est rendu jeudi à Kigali où il a eu des entretiens avec les ministres rwandais des Affaires étrangères et de la Défense sur la situation au Kivu. Il va aussi rencontrer les ambassadeurs de cinq pays membres permanents du conseil de sécurité des Nations unies accrédités à Kigali, pour solliciter l’appui de leurs gouvernements à la Monusco.
Lire aussi sur radiookapi.net:

mardi 24 septembre 2013

Nairobi: les shebab disent "résister"

Dernière mise à jour: 24 septembre, 2013 - 10:55 GMT
Les forces de sécurité kényanes en embuscade, le 23 septembre 2013.
Les islamistes somaliens shebab, qui ont revendiqué l’attaque du Westgate à Nairobi, ont affirmé mardi détenir encore des otages vivants dans le centre commercial.
Sur leur compte Twitter, les insurgés déclarent qu’un nombre “incalculable de cadavres” jonche le sol du bâtiment.
Des tirs sporadiques et des explosions ont été entendus mardi matin, quatre jours après l’attaque qui a fait 62 morts, 170 blessés, et plus d’une cinquantaine de disparus.

Un commandant militaire kényan a déclaré à la BBC qu’il pensait que deux ou trois assaillants pourraient toujours se trouver à l’intérieur du Westland.

Après l’assaut lancé la veille par les forces kényanes, le gouvernement avait déclaré que la situation était “sous contrôle”, et que l'opération était dans sa phase finale.
Selon la police, six assaillants ont été tués pendant la nuit.
"Nos forces passent au peigne fin étage après étage à la recherche des personnes qui auraient été oubliées", a déclaré le porte-parole du gouvernement.

La “veuve blanche” impliquée?

De son coté, la ministre kényane des Affaires étrangères, Amina Mohamed, a déclaré lundi soir sur la chaîne américaine PBS que “deux ou trois” Américains et une femme britannique figuraient parmi les assaillants.
Selon elle, les Américains étaient âgés de 18 ou 19 ans, d’origine arabe ou somalienne, et “vivaient au Minnesota et ailleurs”.
Une photo de Samantha Lewthwaite, dite "la veuve blanche" sur son faux passeport sud-africain en 2011.
La ministre a également déclaré que la Britannique était une femme qui avait “commis des actes similaires à de nombreuses reprises”.
La police kényane avait affirmé plus tôt qu’elle suspectait la Britannique Samantha Lewthwaite, dite la “veuve blanche”, veuve d’un des kamikazes des attentats du 7 juillet 2005 à Londres, d'être impliquée.

Les autorités britanniques ne confirment pas cette hypothèse, et disent attendre la poursuite de l'enquête.
Les shebabs ont démenti la présence d’étrangers parmi les assaillants.